TUNAUONEA FAHARI UFUFUO WA KRISTO
Yohana 11:25-26
Baada ya kusulubiwa kwa Kristo, makuhani na watawala hawakujisikia hisia ya ushindi ambayo waliitegemea. Hawakushangilia mafanikio yao Katika kunyamazisha Sauti ya Mwalimu Mkuu. Waliogopa.Tayari kifo chake kilivutia watu kuyatafakari maisha na tabia yake. Sasa Makuhani walisadiki kwamba walikuwa wameshindwa Katika majaribio yao ya kulipiza kisasi, hivyo sasa wakamwogopa zaidi kristo aliyekufa, zaidi sana, kuliko walivyomwogopa kristo aliyekuwa hai....
Nuru ya Mbinguni ililizunguka kaburi na Mbingu yote ikaangazwa kwa utukufu wa malaika. Malaika alilikaribia kaburi na baada ya kuliviringisha jiwe kana kwamba lilikuwa kokoto, aliketi juu yake. Kisha Sauti yake ikasikika, "Mwana wa Mungu, njoo huku nje; Baba yako anakuita"
Na Yesu akatoka kwenye kaburi kwa mwendo wa mshindi mkuu.kulikuwa na mlipuko wa ushindi, kwani familia ya Mbinguni ilikuwa inasubiri kumpokea; na yule malaika Mkuu, akifuatiwa na jeshi la Mbinguni, aliinama kwa heshima mbele zake Wakati Yeye, Mfalme wa Mbinguni, huku akiwa juu ya kaburi la Yusufu likilokuwa limepasuliwa, alitangaza, "Mimi ndimi huo ufufuo na uzima"
Viumbe wote walioumbwa wanaishi kutokana na mapenzi na nguvu ya Mungu. Wao Ni wapokeaji wa uzima wa Mwana wa Mungu. Hata wakiwa na uwezo na talanta kiasi gani, hata wakiwa na umahiri kiasi gani, huwa wanajazwa upya kwa uzima kutoka kwake aliye chanzo cha uzima wote. Yeye ni chemchemi, Chemchemi ya uzima .... Uzima ambao aliuweka chini Katika ubinadamu, aliutwaa tena na kuwapa binadamu. Alisema,
"Mimi nalikuja ili wawe na uzima, Kisha wawe nao tele"....
Kristio alikuja akawa mmoja pamoja na binadamu, ili ubinadamu upate kuwa Katika umoja na Roho na uzima pamoja naye. Kutokana kuwa na umoja huu Katika kutii Neno la Mungu, maisha yake yanakuwa maisha yao. Anamwambia aliyeungama, "Mimi ndiye huo ufufuo na uzima"





