Alhamisi, 4 Agosti 2016

ASILI YETU
Mwanzo 1:1-8
-Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi-
Pamoja nchi ilikuwa utupu na giza lilitanda juu yake Roho ya Mungu ilitulia juu ya uso wa maji, ndipo Mungu akaanza kutamka iwe nuru, nayo nuru ikawepo
    -Mungu akaona nuru yakuwa ni njema na akatenga nuru na giza, Nuru mchana na giza Usiku. Pia siku hii Mungu alilitenga anga katikati ya maji akaliita anga Mbingu, ikawa asubuhi ikawa jion siku ya kwanza

 Fungu la 10. Mungu akapaita pale pakavu Nchi, makusanyiko ya maji akayaita Bahari. Mungu akaona kuwa ni vyema.
  -akasema na nnchi itoe majani , mche utoao mbegu kwa jinsi yake (yaani tofauti tofauti) na miche izaao matunda ambao mbegu zake zimo ndani yakekwa jinsi yake. Mungu akaona yakuwa ni vyema.

Fungu la 16. Mungu akafanya mianga miwili mikubwa ule mkubwa utawale mchana na mdogo utawale usiku na akafanya na nyota pia.Mungu akaiweka katika anga la mbingu , itie nuru juu ya nchi. kutawala mchana na usiku kutenga nuru na giza.Mungu akaona ni vyema. ikawa asubuhi ikawa jioni siku nne (4)
  
Fungu la 20 na kuendelea inaelezea Uumbaji wa viumbe hai wa majini na ndege warukao juu ya anga wakiwepo na nyangumi  Mungu akavibariki na akasema Zaeni mkaongezeke mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi juu ya nchi.
-Ikawa jioni ikawa asubuhi siku ya tano(5).

Mungu akasema. Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa na nacho kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake.Mungu akaona ni vyema.

Fungu la 26: Mungu anasema na Tumfanye Mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu wakatawale samaki wa baharini na ndege wa angani, wanyama na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
-MUNGU AKAUMBA MTU KWA MFANO WAKE, KWA MFANO WA MUNGU ALIMWUMBA, MWANAMUME NA MWANAMKE ALIWAUMBA.

Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi, nakuitiisha: mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Mwanzo 2:1.
Basi mbingu na nchi zikamalizika na jeshi lake lote.

Maelezo:
-Sisi ni wa thamani mno kwa Mungu wetu aliyetuumba kwa mikono yake mitukufu tofauti na wanyama, ndege na vyote tunavyoviona hapa duniani. Pia tuna wajibu ya kuvitunza vyote tulivyokabidhiwa na Muumbaji wetu.
-Ni wajibu wetu kuilinda miili yetu kwani ina thamani kubwa mmno na tumuombe Mungu atufundishe namna bora ya kuitunza miili yetu ili yesu atakaporudi mara ya pili aikute ikiwa misafi ifaayo kuingia katika mji aliyotuandalia.

MBALIKIWE WOTE KATIKA JINA LA YESU MWOKOZI WETU




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni